NIJUE KWA UFUPI

Jina langu ni Neligwa Boaz Mugittu, mtoto wa tatu katika familia yenye watoto wanne nikiwa mtoto wa kiume pekee. Baba yangu anaitwa BOAZ MUGITTU ambaye kwa sasa ni marehemu tangu atutoke 26/6/1998 na kubaki na mzazi mmoja tu ambaye ni Mama yangu kipenzi aitwaye ESTHER PHILIP NAPUNIGWA ambao wote ni WANYIRAMBA kwa kabila na Wakristo katika dhehebu la LUTHERAN. Dada yangu wa kwanza anaitwa CHRISTOWELLU ambaye naye ana familia yake anayoishi nayo huko BUNJU, dadangu wa pili anajulikana kama WANONDA aliyetangulia mbele ya haki 21/4/2002 na baada ya wao ndio akatokea kidume chao NELIGWA 8/3/1990 ikiwa ni siku ya Wanawake duniani na wa mwisho ni mdogo wangu aitwaye TYATAWELLU. Nyumbani kwetu ni Ukonga Mombasa na ki elimu ni mwanafunzi katika chuo cha MLIMANI nikichukua Stashahada ya Uandishi wa habari. Elimu ya msingi nilimalizia LUPALAMA 'A' iliyopo Iringa au TOSAMAGANGA HOME BOYS, kidato cha nne nimemalizia KINDOROKO iliyopo MOSHI na kidato cha sita ni TUNDURU iliyopo RUVUMA. Shule nyinginezo nilizosoma ni KURASINI iliyopo Temeke jijini Dar, UKONGA iliyopo Ilala jijini Dar na MWANDU ya Iguguno mkoani Singida zote kwa elimu ya msingi na sekondari ni KALENGA iliyopo Iringa na Juhudi iliyopo Dar. Hiyo ni historia yangu kwa ufupi mengine tutazidi kufahamishana. Nawapenda wote

Wednesday, December 5, 2012

Friday, August 5, 2011

UZUNGU NOMA

Upendo ni mzuri na muhimu katika maisha yetu lakini tusitumie upendo huo kuwaumiza na kuwatesa wengine wanaotuonyesha upendo huo kwani mtu akikuonyesha heshima mpe heshima yake na hata kama anakudharau mpe heshima yake kwani itamsaidia yule mtu asiyekupa heshima yako kujidharau mwenyewe na kujiona mjinga. Upendo huu nimependa kuuongelea kutokana na maneno ambayo yana uzito ukiyachukulia uzito na mepesi ukiyafanya yawe mepesi nayo si mengine ni maneno ya kiingereza kama vile dear, baby, honey, sweet n.k kwani siku hizi imekuwa kama fasheni watu kuitana na kuandikiana hivyo ambapo si vibaya bali ubaya hutokea mtu anapochukulia tofauti na haina ya mtu aliyemuita kwa mfano watu wa jinsia mbili tofauti ambao ni marafiki mmoja akimuita mwenzake maneno kama hayo akiwa na maana ya kawaida tu ya mpendwa bali yeye huchukulia kama wachumba na kuanza kutangaza kwa wengine na kujisifia hivyo inashusha thamani ya mtu husika kwa wengine na kuonekana ni malaya endapo wanajua kuwa ana mchumba fulani. Kwa hiyo tuwe makini na maneno haya tusipende kuiga na kuwasingizia watu wakati sivyo walivyo. TAFAKARI