NIJUE KWA UFUPI
Jina langu ni Neligwa Boaz Mugittu, mtoto wa tatu katika familia yenye watoto wanne nikiwa mtoto wa kiume pekee. Baba yangu anaitwa BOAZ MUGITTU ambaye kwa sasa ni marehemu tangu atutoke 26/6/1998 na kubaki na mzazi mmoja tu ambaye ni Mama yangu kipenzi aitwaye ESTHER PHILIP NAPUNIGWA ambao wote ni WANYIRAMBA kwa kabila na Wakristo katika dhehebu la LUTHERAN. Dada yangu wa kwanza anaitwa CHRISTOWELLU ambaye naye ana familia yake anayoishi nayo huko BUNJU, dadangu wa pili anajulikana kama WANONDA aliyetangulia mbele ya haki 21/4/2002 na baada ya wao ndio akatokea kidume chao NELIGWA 8/3/1990 ikiwa ni siku ya Wanawake duniani na wa mwisho ni mdogo wangu aitwaye TYATAWELLU. Nyumbani kwetu ni Ukonga Mombasa na ki elimu ni mwanafunzi katika chuo cha MLIMANI nikichukua Stashahada ya Uandishi wa habari. Elimu ya msingi nilimalizia LUPALAMA 'A' iliyopo Iringa au TOSAMAGANGA HOME BOYS, kidato cha nne nimemalizia KINDOROKO iliyopo MOSHI na kidato cha sita ni TUNDURU iliyopo RUVUMA. Shule nyinginezo nilizosoma ni KURASINI iliyopo Temeke jijini Dar, UKONGA iliyopo Ilala jijini Dar na MWANDU ya Iguguno mkoani Singida zote kwa elimu ya msingi na sekondari ni KALENGA iliyopo Iringa na Juhudi iliyopo Dar. Hiyo ni historia yangu kwa ufupi mengine tutazidi kufahamishana. Nawapenda wote
Tuesday, June 28, 2011
BABA NAKUKUMBUKA
26/6/1988, Ni siku ambayo haitakuja kusahaulika maisha yangu yote hadi pale na mimi nitakapomfuata mtu aliyenitoka siku kama hiyo tena tuliyekuwa tumelala naye kitanda kimoja lakini kazi ya MUNGU haina makosa namwomba yeye atoaye na atwaaye ailaze roho ya baba yangu mpendwa BOAZ MUGITTU mahala pema peponi Amennnnnnnnnnnnnnnnnnnnnn.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment